Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Sisi wote tumepokea sehemu ya neema aliyojaa nayo, akitupatia baraka nyingi sana.

Gade chapit la Kopi




Yoane 1:16
24 Referans Kwoze  

Kwa maana Mungu mwenyewe alitaka ukamilifu wake uonekane ndani ya mwana wake.


Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.


Ni kweli kwamba kifo kilitawala kwa njia ya mutu mumoja, kwa sababu ya kosa la huyo mumoja. Lakini inaonyesha zaidi sana kwamba wale wanaopewa neema ya Mungu kwa uwingi na zawadi ya haki yake, wataishi na kutawala kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


Kwa maana mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine, naye atakuwa na vitu vingi. Lakini mutu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kile kidogo anachokuwa nacho.


kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


Lakini ninyi sasa hamutawaliwi na hali yenu zaifu ya kimwili, lakini munatawaliwa na Roho Mutakatifu, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Na mutu yeyote asiyekuwa na Roho wa Kristo ndani yake, yeye si mutu wa Kristo.


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Lakini Yoane akamukatalia, akimwambia: “Ni mimi ninayepaswa kubatizwa nawe; namna gani unakuja kwangu?”


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alitangulia kushuhudia mateso yatakayomupata Kristo na utukufu utakaokuwa nyuma. Nao walijitolea kusudi wapate kuvumbua wakati gani na kwa njia gani mambo haya yatafanyika.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka, wanalifanya kuwa chemichemi, nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite