Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yeremia 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.

Gade chapit la Kopi




Yeremia 1:2
18 Referans Kwoze  

Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.


Neno la Yawe lilimufikia Yona mwana wa Amitai kusema hivi:


Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Yeremia, unaona nini? Nami nikasema: Ninaona tawi la muti wa uangalivu ambao maua yake yamekwisha kuchanua.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Walipokuwa kwa meza, neno la Yawe lilimufikia yule nabii muzee


Twaa kizingo cha kitabu uandike humo maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, juu ya Yuda na mataifa yote, tangu siku nilipoanza kusema nawe, wakati Yosia alipokuwa mufalme mpaka leo.


Kwa muda wa miaka makumi mbili na tatu sasa, ni kusema tangu mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa mufalme Yosia, mufalme wa Yuda, mwana wa Amoni, mpaka hivi leo, nimekuwa nikipata neno la Mungu na kulitoa kwenu kila wakati, lakini ninyi hamukusikiliza.


Lakini watu wa Yuda wakawaua wote waliomwua Amoni. Kisha watu hao wa Yuda wakamuweka mwana wake Yosia kuwa mufalme kwa pahali pake.


Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Manase akakufa na kuzikwa katika bustani ya nyumba yake mwenyewe, katika Bustani ya Uza. Naye mwana wake Amoni akatawala kwa pahali pake.


Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, mufalme alimutuma Safanu mwana wa Azalia, mujukuu wa Mesulamu, mwandishi katika nyumba ya Yawe akisema:


Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!


Nyuma ya pale nabii Hanania alipovunja nira kutoka katika shingo la nabii Yeremia, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:


Hili ni neno la Yawe lililomufikia Yoeli mwana wa Petueli.


Hili ni neno la Yawe lililomufikia Zefania mwana wa Kusi, mujukuu wa Gedalia mwana wa Amaria, wa uzao wa mufalme Hezekia, wakati wa utawala wa mufalme Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite