Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”
Lakini wewe Yawe uko pamoja nami. Kwangu wewe ni kama shujaa wa kutisha. Kwa hiyo watesaji wangu watajikwaa, nao hawataweza kunishinda. Watafezeheka kabisa, kwa sababu hawatashinda. Haya yao itadumu hata milele, nayo haitasahauliwa.
Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.
Lakini musimwasi tu Yawe, wala musiwaogope wenyeji wa inchi hiyo. Maana wao ni kama mboga tu kwetu. Kingo yao imekwisha kuondolewa kwao naye Yawe yuko pamoja nasi. Musiwaogope!
Na tangu leo, ninakufanya kuwa imara kama muji unaozungukwa na kuta, kama munara wa chuma na kama ukuta mugumu sana wa shaba. Utakuwa na nguvu juu ya inchi yote, juu ya wafalme wa Yuda, wakubwa wake, makuhani wake na watu wake wote.
Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo nimekutawanya kati yao, lakini wewe sitakuangamiza. Nitakuazibu kadiri unavyostahili, sitakuacha bila kukuazibu.
Kisha akauliza: Lakini sasa mbona ninaona watu wane wakitembeatembea mule ndani ya moto bila kufungwa na wala hawaunguwi, na mutu wa ine anaonekana kama mwana wa miungu?
Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.
Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.
Basi Yeremia alipomaliza kutangaza mambo yote ambayo Yawe aliyomwamuru kutangaza kwa watu wote, makuhani, manabii na watu wote walimukamata na kusema: Wewe unapaswa kuuawa!