Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yeremia 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Maana ninaziita falme zote na makabila yote ya kaskazini. Wafalme wake wote watakuja na kila mumoja wao ataweka kiti chake cha kifalme mbele ya milango ya ukuta wa Yerusalema na kandokando ya kuta zake zote, na kuizunguka miji yote ya Yuda.

Gade chapit la Kopi




Yeremia 1:15
24 Referans Kwoze  

Kisha uwaambie hivi: Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Muangalie, mimi nitamutuma na kumuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mutumishi wangu, naye ataweka kiti chake cha kifalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha hapa, na kutandaza paa la kifalme juu yake.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Inayaarifu mataifa, inaitangazia Yerusalema maneno haya: Washambulizi wanakuja kutoka inchi ya mbali, wanaitisha miji ya Yuda,


(Basi wakubwa hawa wote wa mufalme wa Babeli waliingia na kukaa kwenye mulango wa katikati: Nergali-Sarezeri, Samgari-Nebo, Sarsekimu jemadari mukubwa wa na Nergali-Sarezeri mukubwa wenye maarifa, pamoja na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babeli.)


Umwange hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu, na juu ya watu ambao hawakutambui. Maana, wamewaua wazao wa Yakobo; wamewaua na kuwaangamiza kabisa, na inchi yao wameiacha mabomoko.


Mabonde yako mazuri, ewe Yerusalema, yalijaa magari ya vita na farasi; wapanda-farasi walijipanga tayari kwenye milango yako.


Wanawake wetu wanatendewa kwa kinguvu katika Sayuni, na wabinti wetu katika miji ya Yuda.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Nitawaamuru nao wataurudia katika muji huu. Wataushambulia, watauteka na kuuteketeza kwa moto. Nitaifanya miji ya inchi ya Yuda kuwa ukiwa bila wakaaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


Kama wakikataa kukipokea kikombe hicho utakachowapatia kwa kunywa, utasema hivi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Ni lazima mukunywe!


Musikilize ile fujo! Angalia inakuja. Kunatokea shindo kubwa upande wa kaskazini. Taifa kutoka kaskazini linakuja kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwa, wataigeuza mapango ya mbweha!


Yawe anasema hivi: Muangalie, watu wanakuja toka inchi ya kaskazini; taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali kwa mwisho wa dunia.


Na kwa ngambo yenu ninyi watu wa Israeli, ninaleta taifa moja kutoka mbali kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hili taifa haliwezi kushindwa, ni taifa la zamani, ni taifa ambalo hamufahamu luga yake. Hamuwezi kuelewa hata neno wanalolisema.


Muinue bendera ya vita kuelekea Sayuni, kusudi mukimbie, wala musisitesite! Yawe analeta hasara, analeta maangamizi makubwa kutoka kaskazini.


Inua macho yako, ee Yerusalema! Angalia! Waadui zako wanakuja kutoka kaskazini. Kundi ulilopewa liko wapi? Kundi lako zuri liko wapi?


Yawe akamutolea Yeremia ujumbe huu wakati Nebukadneza, mufalme wa Babeli, pamoja na waaskari wake wote na falme zote za dunia zilizokuwa chini ya utawala wake, vilevile na watu wote walipokuwa wakiushambulia Yerusalema na miji mingine yote ya kandokando yake:


Watu wa Misri watapata haya, watatiwa katika mikono ya watu kutoka kaskazini.


Wakubwa wote wa watu wa upande wa kaskazini wako huko vilevile; hata Wasidoni wote walikwenda kujiunga na wafu. Walipokuwa wangali wanaishi, walisababisha vitisho kwa nguvu zao, lakini sasa hao wasiomujua Mungu wamelalishwa chini na haya pamoja na wale waliouawa katika vita. Wanashiriki haya ya wale walioshuka ndani ya shimo kwa wafu.


Nitawaondoa hao waadui wanaotoka kaskazini, nitawafukuza mpaka katika jangwa; waaskari wa mbele nitawatupa katika bahari ya Chumvi na wale wa nyuma katika bahari ya Mediteranea. Watatoa uvundo na harufu mbaya, hao ambao wamefanya maovu makubwa.


Lile gari linalokokotwa na farasi weusi linakwenda upande wa kaskazini, lile linalokokotwa na farasi weupe linakwenda upande wa magaribi, na lile linalokokotwa na farasi wa kijivujivu linakwenda upande wa kusini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite