Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yeremia 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Yawe akaniambia: Maangamizi yataanzia tokea kaskazini na kuwapata wakaaji wote wa inchi hii.

Gade chapit la Kopi




Yeremia 1:14
17 Referans Kwoze  

Musikilize ile fujo! Angalia inakuja. Kunatokea shindo kubwa upande wa kaskazini. Taifa kutoka kaskazini linakuja kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwa, wataigeuza mapango ya mbweha!


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Muinue bendera ya vita kuelekea Sayuni, kusudi mukimbie, wala musisitesite! Yawe analeta hasara, analeta maangamizi makubwa kutoka kaskazini.


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Nilipoangalia niliona upepo wa zoruba unavuma kutokea upande wa kaskazini: kulikuwa wingu kubwa lililozungukwa na mwangaza, na moto ulitokea humo mufululizo na katikati ya huo moto kulikuwa kitu kinachometameta kama shaba.


Muangalie! Watu wanakuja toka inchi ya kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi linajitayarisha kutoka mbali kwa miisho ya dunia.


Maana, mimi nitachochea mataifa makubwa kutoka inchi ya kaskazini washambulie inchi ya Babeli. Watajitayarisha kuishambulia inchi ya Babeli na kuiteka. Mishale yao ni kama shujaa hodari asiyerudi mikono mitupu.


Misri ni kama mwana-ngombe muzuri, lakini uharibifu kutoka kaskazini umekuja juu yake.


Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini, nitawakusanya kutoka miisho ya dunia. Wote watakuwa pale; hata vipofu na vilema, wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa; kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.


Yawe anasema hivi: Muangalie, watu wanakuja toka inchi ya kaskazini; taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali kwa mwisho wa dunia.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


Mimi Yawe wa majeshi niliuotesha huu muzeituni; lakini sasa ninatangaza hasara juu yake, kwa sababu ya maovu ambayo watu wa Israeli na Yuda wameyafanya. Wamenikasirikisha kwa kumufukizia mungu Bali ubani.


Yawe anasema hivi: Maji yanapanda kutoka kaskazini, nayo yatakuwa muto uliofurika; yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake, muji na wakaaji na wanaoishi humo. Watu watalia, wakaaji wote wa inchi wataomboleza.


Uwape mufano hao watu wangu waasi na kuwaambia kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Weka chungu juu ya mafika, ukijaze maji vilevile.


Nitawaondoa hao waadui wanaotoka kaskazini, nitawafukuza mpaka katika jangwa; waaskari wa mbele nitawatupa katika bahari ya Chumvi na wale wa nyuma katika bahari ya Mediteranea. Watatoa uvundo na harufu mbaya, hao ambao wamefanya maovu makubwa.


Lile gari linalokokotwa na farasi weusi linakwenda upande wa kaskazini, lile linalokokotwa na farasi weupe linakwenda upande wa magaribi, na lile linalokokotwa na farasi wa kijivujivu linakwenda upande wa kusini.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite