Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!

Gade chapit la Kopi




Yakobo 5:9
21 Referans Kwoze  

Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.


Vilevile, wakati mutakapoona mambo haya yote niliyotoka kutaja yanatokea, mujue kwamba yeye yuko karibu, na amekuwa kwa mulango.


Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.


Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


Lakini watu hawa watasamba maneno yao mbele ya Mungu anayekwisha kuwa tayari kwa kuhukumu wafu na wazima.


Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”


Mambo haya yote yaliwafikia kusudi yakuwe mufano kwa watu wengine; yameandikwa kwa kutuonya sisi, kwa maana tunaishi katika kipindi cha mwisho wa nyakati.


Vilevile, wakati mutakapoona mambo hayo niliyotoka kutaja yanatokea, mujue kwamba yeye yuko karibu, na amekuwa kwa mulango.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


Kwa hiyo Herodia akamuwekea Yoane chuki na kutaka kumwua, lakini hakuweza kwa sababu ya Herode.


Kila magaribi waadui hao wanarudi wakifoka kama imbwa, na kuzungukazunguka katika muji.


Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.


Wakati umetimia, ile siku imekaribia. Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze; kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.


Mungu peke yake ndiye anayesimamisha Sheria na anayeweza kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi wewe unayemuhukumu mwenzako, unajizania kuwa nani?


Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha.


Wandugu zangu, mukumbuke manabii waliotabiri kwa jina la Bwana, muangalie namna walivyovumilia katika mateso, nanyi mufuate mufano wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite