Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nanyi vilevile, muvumilie na kutia mioyo yenu nguvu, kwa maana Bwana yuko karibu kurudi.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 5:8
24 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Muonyeshe upole wenu kwa watu wote, kwa maana Bwana yuko karibu kurudia.


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Mwenye kushuhudia maneno hayo anasema: “Ndiyo, ninakuja upesi!” Amina! Kuja Ee Bwana Yesu!


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Ninamutumainia Yawe kwa moyo wangu wote. Ninaaminia sana neno lake.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


“Ee Yawe, ninangojea uniokoe!


Wakati umetimia, ile siku imekaribia. Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze; kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.


Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”


Yesu akamujibu: “Ikiwa ninataka huyu aishi mpaka nitakaporudi, jambo hili halikuangalii! Wewe, unifuate!”


Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.


Zahabu na feza yenu vimepata kutu. Na kutu hii ndiyo itakayowashitaki, nayo itateketeza mwili wenu kama vile moto. Mumejiwekea akiba katika siku hizi za mwisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite