Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kati yenu kuna mutu anayekuwa katika mateso? Aombe kwa Mungu. Au kuna mutu anayekuwa katika furaha? Aimbe nyimbo za sifa.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 5:13
34 Referans Kwoze  

Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Munapoongea, museme maneno ya zaburi, mumusifu Bwana na kumwabudu kwa nyimbo za kiroho. Mumwimbie na kumushangilia kwa moyo wenu wote.


Basi, Yona akiwa ndani ya tumbo la samaki yule, akamwomba Yawe Mungu wake,


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Niliteremuka mpaka kwenye misingi ya milima, katika inchi ambayo milango yake imefungwa milele. Lakini wewe, ee Yawe, Mungu wangu, umenipandisha nikiwa muzima kutoka mule ndani ya shimo.


Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.


Wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliimba wimbo mupya mbele ya kile kiti cha kifalme na mbele ya vile viumbe vine vya ajabu na ya wale wazee. Hakuna mutu aliyeweza kujifunza wimbo ule, isipokuwa wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliokombolewa katika dunia.


Yesu alikuwa katika uchungu mukubwa, akazidi kuomba kwa bidii. Jasho iliyomutoka ikakuwa kama matone ya damu yaliyokuwa yakitiririka mpaka chini.]


Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.


Katika taabu yangu nilimwomba Yawe, naye akanisikia na kuniweka huru.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Nao walilalamika hivi kwa sauti kubwa: “Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo!”


Wandugu zangu, niseme nini basi? Wakati munapokusanyika kwa ibada, mumoja anaweza kuimba wimbo, mwingine kufundisha, mwingine kutoa ufunuo, mwingine kusema kwa luga za ajabu na mwingine anaweza kutafsiri. Na hayo yote yanapaswa kufanyika katika nia ya kujenga kanisa katika imani.


Na akaongeza kusema: “Ee Yesu, usinisahau wakati utakapokuja katika ufalme wako!”


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Mushangilie, mumwimbie Mungu sifa, mueleze matendo yake ya ajabu!


Tuende mbele yake na nyimbo za shukrani; tumushangilie kwa nyimbo za sifa.


kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya kifo ilikuwa mbele yangu.


Kisha atamwomba Mungu na kukubaliwa, atakuja mbele yake kwa furaha, na Mungu atamurudishia utukufu wake.


Mushangilie, mumwimbie Mungu sifa; mueleze matendo yake ya ajabu!


Watumishi wangu wataimba kwa furaha ndani ya moyo, lakini ninyi mutalia kwa uchungu ndani ya moyo na kupiga kelele kwa uchungu mukubwa ndani ya roho.


Basi ninapaswa kufanya nini? Nitaomba katika roho na katika akili vilevile. Nitaimba katika roho na katika akili vilevile.


Wandugu zangu, mukumbuke manabii waliotabiri kwa jina la Bwana, muangalie namna walivyovumilia katika mateso, nanyi mufuate mufano wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite