Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 5:11
53 Referans Kwoze  

Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena: Yawe, Yawe, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa wema na uaminifu.


Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Akamujibu: “Wewe unasema kama wanawake wapumbafu. Tukipokea mazuri kutoka kwa Mungu, kwa nini tukatae kupokea vilevile mabaya kutoka kwake?” Katika mambo hayo yote, Yobu hakusema neno lolote la kumukosea Mungu.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Mukuwe wenye huruma, kama vile Baba yenu anavyokuwa mwenye huruma.


Wema wa Yawe haukomi, huruma zake hazina mwisho.


Yawe ni mwenye rehema na huruma; ni muvumilivu na mwingi wa wema.


“Mimi Yawe si mwepesi wa hasira, ni mwenye wema mwingi, na ni mwenye kusamehe uovu na makosa. Lakini kwa vyovyote vile sitakosa kuwaazibu watoto na wajukuu mpaka kizazi cha tatu na cha ine kwa zambi za wazazi wao.”


Lakini sisi si watu wenye kurudi nyuma na kupotea, lakini sisi ni watu wenye imani na wenye kuokoka.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa upendo wake mukubwa;


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Daudi akamujibu Gadi: “Nimeingia katika mashaka makubwa! Lakini afazali niazibiwe na Yawe maana yeye ana huruma sana. Lakini nisianguke katika mukono wa mwanadamu.”


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Au haujali na uwingi wa wema, utulivu na uvumilivu wa Mungu? Haujui kwamba wema wake ungeweza kukuongoza hata upate kugeuka toka zambi?


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Kwa hiyo akaomba: Yawe, si hayo ndiyo mambo yaleyale niliyowaza utayafanya nilipokuwa katika inchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka kukimbilia Tarsisi. Nilijua kwamba wewe ni Mungu ambaye umejaa huruma na rehema, haukasiriki upesi, wewe ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia yako kusudi usiazibu.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Mwisho wa jambo ni afazali kuliko mwanzo wake. Moyo muvumilivu ni bora kuliko moyo wa majivuno.


Unigeukie na kunionea huruma, kama unavyowatendea wanaokupenda.


Yawe ni mwenye huruma na haki; Mungu wetu ni mwenye rehema.


Kama vile baba anavyohurumia mwana wake, ndivyo Yawe anavyohurumia wote wanaomwabudu.


Heri mutu unayemwadibisha, ee Yawe, mutu unayefundisha sheria yako,


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Muangalie mutu mukamilifu, mutu wa usawa; mutu anayependa amani anajaliwa wazao.


Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.


Yobu alikuwa na wana saba na wabinti watatu.


Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia


Mukimurudilia Yawe, wale ambao walipeleka wandugu zenu na watoto wenu kuwa wafungwa, watawahurumia na kuwaacha warudi katika inchi hii. Kwa maana Yawe, Mungu wenu, ni mwenye huruma na rehema, naye hatawageuzia mugongo ikiwa mutamurudilia.”


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


Yawe ni mwenye huruma na rehema; yeye hakasiriki upesi, amejaa wema.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.


Hata hivyo, kutokana na rehema zako nyingi, haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia, maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.


Kulikuwa mutu mumoja katika inchi ya Usi, aliyeitwa Yobu. Mutu yule alikuwa mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.


Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali,


Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.


Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite