Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wandugu zangu, mukumbuke manabii waliotabiri kwa jina la Bwana, muangalie namna walivyovumilia katika mateso, nanyi mufuate mufano wao.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 5:10
19 Referans Kwoze  

Muwakumbuke waongozi wenu waliowatangazia neno la Mungu. Muangalie vizuri namna walivyoishi na kufa. Mufuate imani yao.


Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.


Yeye anapaswa kubaki mbinguni mpaka zitakapotimia zile nyakati Mungu atakapotengeneza vitu vyote sawa vile alivyosema tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake watakatifu.


Mambo hayo yatakapotokea, mufurahi na kurukaruka, maana munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi babu zao walivyowatendea manabii.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Naye Hezekia akamwambia Isaya: Neno la Yawe ulilosema ni zuri. Alisema hivyo maana alifikiri: Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Basi wakubwa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii: Mutu huyu hastahili hukumu ya kifo. Amesema nasi kwa jina la Yawe, Mungu wetu.


Kama wangalihuzuria katika baraza langu, wangalitangazia watu wangu maneno yangu, wangaliwageuza kutoka katika njia zao mbaya, na kutoka katika matendo yao maovu.


Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.


Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha.


Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Kati yenu kuna mutu anayekuwa katika mateso? Aombe kwa Mungu. Au kuna mutu anayekuwa katika furaha? Aimbe nyimbo za sifa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite