Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Munatamani kupata kitu fulani, lakini hamukipati. Munaua na kusikia wivu, lakini hamuwezi kupata kitu. Na kwa hiyo, munagombana na kuwa na ugomvi. Hamupati kitu munachotaka kwa sababu hamukiombi kwa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 4:2
14 Referans Kwoze  

Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.


Zaidi ya hayo, divai inapotosha; mutu mwenye kiburi hatadumu. Yuko tayari kuwameza wengine kama kuzimu; kama vile kifo, hatosheki na kitu. Anajikusanyia mataifa yote, na watu wote kama mali yake.


Ahazi akajibu: Sitaomba kitambulisho! Sitaki kumujaribu Yawe.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Mumewahukumu na kuwaua wenye haki, nao hawakupingana nanyi.


Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni mwuaji, nanyi munajua kwamba mwuaji yeyote hana uzima wa milele ndani yake.


Naye akamwambia: “Kwa sababu nilizungumuza na Naboti wa Yezereheli, nikataka aniuzishie shamba lake la mizabibu, au kama akipenda nimupe shamba lingine pahali pa lile. Lakini yeye akaniambia: ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite