Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 4:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Basi, mutu anayejua kutenda mema wala hayatendi, anafanya zambi.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 4:17
9 Referans Kwoze  

Yesu akawajibu: “Mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini kwa maana munajidai kwamba munaona, mungali katika zambi.”


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Kama singekuja kusema nao, wasingekuwa na zambi; lakini sasa hawataweza kukana zambi yao.


Maana ingekuwa heri kwao kama wasingejua njia ya haki, kuliko kuijua na kisha kuacha ile amri takatifu waliyopewa.


Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.


Basi ni kusema kile kinachokuwa kizuri kimeniletea kifo? Hapana hata kidogo! Ni zambi ndiyo iliyoniletea kifo. Lakini kusudi zambi ionekane kuwa zambi kweli kweli, ilipitia kwa njia ya kile kinachokuwa kizuri kwa kusababisha kifo changu. Hivi kwa njia ya amri ile, zambi ilizidi kujikamilisha kuwa zambi kabisa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite