Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 3:2
29 Referans Kwoze  

Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.


Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Kuna mutu anayependa kuishi vizuri, na kukaa katika siku za heri? Azuize ulimi wake na mabaya nayo midomo yake na uongo.


Kwa maana kila mutu atapata sheria au kupata azabu kufuatana na maneno yake.”


Unatamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mazuri?


Nani anayesubutu kusema: “Nimetakasa moyo wangu; mimi nimetakasika na zambi yangu?”


Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.


Ni sawa ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Hakuna hata mutu mumoja mwenye haki!


Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.


“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, nawe ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na adui, hata wapelekwe mateka mpaka katika inchi ya adui inayokuwa mbali au karibu,


Kwa maana mutu akivunja agizo moja tu la Sheria, yeye anavunja Sheria yote.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Lakini ninatesa mwili wangu kwa mazoezi makali na kuutumikisha vikali kusudi mimi mwenyewe nisikataliwe kisha kutangaza ujumbe kwa watu wengine.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.


Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.


Basi ninatambua kanuni hii: wakati ninapotaka kufanya jambo jema, mara moja ninavutwa kufanya jambo baya.


“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, na ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na waadui, hata wapelekwe kuwa watumwa mpaka inchi ya mbali au ya karibu,


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.


Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.


Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.


kuhani atamwangalia mutu yule. Ikiwa kuhani ataona kwamba alama hizo ni nyeupe kidogo, huo ni upele wa kawaida, mutu yule ni safi.


hata kumwasi Mungu na kusema maneno mabaya kama yale?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite