Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 2:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?

Gade chapit la Kopi




Yakobo 2:20
16 Referans Kwoze  

Kwa maana kama vile mwili usiokuwa na pumzi ndani yake umekufa, hivi vilevile imani pasipo matendo imekufa.


Ni hivi vilevile, imani peke yake pasipo matendo imekufa kabisa.


Mulimaji mwenye bidii ana chakula tele, lakini anayefuata mambo yasiyofaa hana akili.


Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.


Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.


Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.


Kufuatana na hiyo, kuna watu wengi hasa kati ya Wayuda walioamini, wanaokuwa waasi, wakatetea na wadanganyifu.


Watu wamoja wamekosa kuwa na tabia hiyo hata wamefuata maneno ya ovyo ovyo.


Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Kwa maana tunaona kama mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani wala si kwa njia ya kutii Sheria.


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite