Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi museme na kutenda kama watu watakaohukumiwa kufuatana na sheria inayotuweka kuwa huru.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 2:12
8 Referans Kwoze  

Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.


Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


“Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,


Halafu mutajua ukweli, na ukweli utawaweka huru.”


Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite