Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 kwa sababu ni mutu wa nia mbili, na mwenye kugeukageuka katika mwenendo wake.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 1:8
13 Referans Kwoze  

Kisha, Elia akawakaribia watu hao, akawaambia: “Mutaendelea kusitasita ndani ya mioyo mpaka wakati gani? Ikiwa Yawe ni Mungu, mumufuate; lakini ikiwa Bali ni Mungu, basi, mumufuate.” Lakini watu hawakumujibu neno lolote.


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Basi mataifa haya yalimwabudu Yawe, lakini vilevile walitumikia sanamu zao za madini yenye kuyeyushwa; na mpaka sasa hivi, wazao wao wanaendelea kutenda hivyo kama vile babu zao walivyotenda.


Ni vile ndivyo alivyoandika katika barua zote alimosema ndani yao juu ya mambo yale. Lakini ndani ya barua zile kunakuwa mambo mengine magumu kuyasikia. Na watu wajinga na wasiokamilika wanageuzageuza maana yake sawa vile wanavyogeuza sehemu zingine za Maandiko Matakatifu. Kwa njia ile wanajiangamiza wenyewe.


Hivi wakamwabudu Yawe, lakini wakati uleule wakiwaabudu vilevile miungu yao waliyoleta kutoka inchi zao.


Mioyo yao imejaa udanganyifu. Sasa ni lazima wabebe makosa yao. Yawe atabomoa mazabahu zao na kuziharibu nguzo zao.


“Macho ni taa ya mwili. Kama macho yako yakiwa mazima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza.


Ninachukia watu wanafiki, lakini ninapenda sheria yako.


Mutu wa namna hiyo asizani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Bwana,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite