Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yakobo 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 na ndugu anayekuwa tajiri afurahi kwa sababu Mungu anamushusha. Maana tajiri atatoweka kama maua ya pori.

Gade chapit la Kopi




Yakobo 1:10
19 Referans Kwoze  

Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.


Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.


Anachanua kama maua, kisha ananyauka. Anakimbia kama kivuli na kutoweka.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!


Wale wanaotumia mali ya dunia hii wakuwe kama vile wasioitumia. Kwa maana dunia hii inakaribia kupita.


Maisha ya mwanadamu ni kama majani tu, yanachanua kama maua:


Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.


Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sauti inasema: Tangaza! Nami nikauliza: Nitangaze nini? Naye: Tangaza: wanadamu wote ni kama majani; usitawi wao ni kama maua ya shamba.


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


kwa sababu ya kasirani na hasira yako, maana umeniokota na kunitupilia mbali.


Maana hao watatoweka mara moja kama nyasi; watanyauka kama majani.


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Majani yananyauka na maua yanafifia, Yawe anapovumisha upepo juu yake. Hakika wanadamu ni kama majani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite