Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waroma 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3-4 Habari hiyo inaelekea Mwana wake ndiye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alizaliwa kimwili katika uzao wa mufalme Daudi. Lakini kwa namna ya Roho Mutakatifu, alihakikishwa kwa uwezo kuwa yeye ni Mwana wa Mungu kwa njia ya kufufuka kwake.

Gade chapit la Kopi




Waroma 1:3
66 Referans Kwoze  

Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Basi, ndivyo inavyokuwa vilevile: sitawatupa wazao wa Yakobo na Daudi, mutumishi wangu; nitamuchagua mumoja kati ya wazao wake atawale wazao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawarudishia tena hali yao na kuwahurumia.


Umukumbuke Yesu Kristo aliyekuwa wa ukoo wa mufalme Daudi, na aliyefufuka sawa vile inavyotangazwa na Habari Njema hii ninayohubiri.


Mungu ni mwaminifu katika ahadi zake, yeye aliyewaita ninyi muishi katika ushirika pamoja na Mwana wake Yesu Kristo, Bwana wetu.


Lakini kwa sababu alikuwa nabii, alijua kwamba Mungu amemwahidi kwa kiapo kwamba atamutawalisha mumoja wa wazao wake kwa kurizi ufalme wake.


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Ametuletea Mwokozi mwenye uwezo, toka ukoo wa mutumishi wake Daudi.


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Mwanamuke mumoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: “Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo.”


Na kundi lote la watu waliokuwa pale wakashangaa na kusema: “Huyu anaweza kuwa kweli Mwana wa Daudi?”


Yesu akaondoka toka pale, naye alipokuwa katika njia, vipofu wawili wakamufuata wakilalamika, wakisema: “Utuhurumie, Ee Mwana wa Daudi!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


“Umwandikie malaika wa kanisa la Tuatera hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa Mwana wa Mungu, anayekuwa na macho yanayometameta kama ndimi za moto, na miguu inayongaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana.


Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Ni nani anayeshinda dunia? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


Kila mutu anayesema kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaungana naye, na mutu yule anaungana na Mungu.


Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Mungu ambaye ninamwabudu kwa roho yangu yote kwa njia ya kutangaza Habari Njema ya Mwana wake, ni mushuhuda wangu kwamba ninawakumbuka siku zote


Na bila kukawia akaanza kuhubiri katika nyumba za kuabudia, akitangaza kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Walipokuwa wakiendelea na safari, wakafika kwenye nafasi moja kwenye maji, yule mukubwa akasema: “Hapa kuna maji. Ni kitu gani kinachonizuiza nisibatizwe?” [


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Maandiko Matakatifu hayakusema kwamba Kristo atazaliwa katika ukoo wa mufalme Daudi na katika muji Betelehemu, pahali Daudi alipoishi?”


Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”


Basi tuseme nini juu ya babu yetu Abrahamu? Nini iliyomutokea?


Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,


Muangalie mufano wa Waisraeli: wale wanaokula vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu wanaungana na Mungu kwa njia ya sadaka ile.


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite