Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Musa akawaambia: Hili ndilo jambo ambalo Yawe aliwaamuru mulifanye kusudi utukufu wake uonekane kwenu.

Gade chapit la Kopi




Walawi 9:6
9 Referans Kwoze  

Halafu Musa na Haruni wakaingia ndani ya hema la mukutano; walipotoka wakawabariki watu, nao utukufu wa Yawe ukaonekana kwa watu wote.


Utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea upande wa mashariki. Pamoja nao kulikuwa mushindo wa kuja kwake kama mushindo wa maji mengi, inchi ilingaa kwa utukufu wake.


Utukufu wa Yawe ukatua juu ya mulima Sinai na wingu likafunika mulima kwa muda wa siku sita. Siku ya saba Mungu akamwita Musa kutoka katikati ya lile wingu.


Wakati Haruni alipokuwa akizungumuza na Waisraeli wote pamoja, watu wote wakaangalia kule katika jangwa na mara moja utukufu wa Yawe ukaonekana katika mawingu.


Waisraeli wakaleta vyote hivyo mbele ya hema la mukutano kama vile Musa alivyowaamuru na wote pamoja wakaenda kusimama mbele ya Yawe.


Hapo ndipo nitakapokutana na Waisraeli na utukufu wangu utapafanya pawe patakatifu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite