Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Musa akamwambia Haruni: Twaa mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, nyama wote wasikuwe na kilema. Kisha uwatoe sadaka mbele ya Yawe.

Gade chapit la Kopi




Walawi 9:2
15 Referans Kwoze  

Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kisha, Musa akaleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.


Kisha Musa akaleta ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, naye Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe huyo.


Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


Na kwa sababu yeye mwenyewe ni muzaifu, anapaswa kutolea sadaka, si kwa sababu ya zambi za watu tu, lakini kwa sababu ya zambi zake mwenyewe vilevile.


Uwaambie Waisraeli watwae beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi, na mwana-ngombe mumoja na mwana-kondoo mumoja wote wa umri wa mwaka mumoja na wasiokuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,


Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Haruni ataingia Pahali Patakatifu akiwa na ngombe dume muchanga kwa ajili ya sadaka ya zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.


Atatwaa kutoka watu wa Israeli beberu wawili kwa ajili ya sadaka ya zambi na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite