Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Vilevile Musa akamupakaa Haruni mafuta juu ya kichwa kwa kumutakasa.

Gade chapit la Kopi




Walawi 8:12
9 Referans Kwoze  

Kisha umupakae Haruni mafuta na wana wake na kuwatakasa kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Ni kama mafuta mazuri yanayotiririka juu ya kichwa, mpaka kwenye ndevu za Haruni, mpaka juu ya upindo wa nguo yake kwenye shingo.


Kisha kufanya hivyo, utatwaa yale mafuta ya kupakaa, umumiminie Haruni juu ya kichwa chake kwa kumutakasa.


Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.


Utamuvalisha ndugu yako Haruni na wana wake nguo zile, kisha uwapakae mafuta na kuwawekea mikono kwa kuwatakasa wanitumikie kama vile makuhani.


Walipotakaswa kwa kupakwa mafuta, Yawe aliamuru Waisraeli wawape sehemu hiyo ya sadaka; hiyo itakuwa siku zote haki yao.


Halafu Musa akatwaa mafuta ya kupakaa na damu kutoka mazabahu akamunyunyizia Haruni na wana wake hata na nguo zao vilevile. Hivyo Musa akamutakasa Haruni na wana wake pamoja na nguo zao.


Musitoke inje ya mulango wa hema la mukutano, kama sivyo mutakufa. Maana mafuta ya kupakaa ya Yawe yangali juu yenu. Haruni na wana wake wakafanya kama vile Musa alivyosema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite