Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ikiwa mutu anatoa sadaka hiyo kwa kumushukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta.

Gade chapit la Kopi




Walawi 7:12
25 Referans Kwoze  

Vilevile atatoa kikapu cha mikate isiyotiwa chachu: maandazi ya unga laini na mafuta, na mikate myembamba iliyopakwa mafuta pamoja na sadaka za vyakula na za kinywaji.


Kama mutu anamutolea Mungu sadaka ya ngano iliyochomwa kwenye furu, hiyo itakuwa ya mikate isiyotiwa chachu ya unga laini uliochanganywa na mafuta ya zeituni, au ya mikate myembamba isiyokuwa na chachu na isiyopakwa mafuta.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.


Mumushukuru Mungu Baba siku zote kwa kila jambo, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.


Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.


Hakuna mwingine kati yao aliyerudia kwa kumutolea Mungu shukrani, isipokuwa huyu mugeni tu?”


Akainama uso mpaka chini mbele ya Yesu na kumushukuru. Mutu huyo alikuwa Musamaria.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Nitakutolea sadaka za shukrani. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Anayenitolea shukrani kama sadaka yake, huyo ndiye anayenitukuza; yeyote anayedumu katika njia yangu, huyo ndiye nitakayemwokoa.”


Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.


Akarudisha mazabahu ya kumwabudia Yawe, na juu yake akatoa sadaka za amani na za shukrani, akawaamuru watu wa inchi ya Yuda wamwabudu Yawe, Mungu wa Israeli.


Halafu Hezekia akawaambia watu: “Sasa mumekwisha kujitakasa, mukaribie, mulete sadaka na matoleo ya shukrani katika nyumba ya Yawe.” Basi, watu wakaleta sadaka zao na matoleo yao ya shukrani, na za kuteketeza.


Utakaponitolea mimi Yawe sadaka ya shukrani utaitoa kwa namna ambayo itakufanya ukubaliwe.


Nyama ya sadaka hiyo ya amani ya kumushukuru Mungu itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa. Hataacha hata sehemu yake mpaka asubui.


Sadaka yoyote ya ngano iliyotolewa na kuhani itateketezwa yote; haitakuliwa hata kidogo.


Ikiwa sadaka unayotoa ni ya mukate uliokaangwa kwenye kikaango, hiyo itakuwa ya unga laini uliochanganywa na mafuta ya zeituni lakini bila chachu.


Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite