Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Moto wa mazabahu lazima uendelee kuwaka wala usizimike. Kila siku asubui kuhani ataweka kuni kwenye moto huo na juu yake atapanga sadaka ya kuteketezwa, mbele ya kuteketeza mafuta ya sadaka ya amani.

Gade chapit la Kopi




Walawi 6:5
16 Referans Kwoze  

Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Naye anapaswa kumurudishia yule masikini mwana-kondoo yule, tena mara ine, maana ametenda jambo baya na hakukuwa na huruma!”


Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”


Mutu akimupatia mwenzake punda, ngombe, kondoo au nyama mwingine yeyote amutunzie na nyama yule akikufa au akipelekwa bila mutu yeyote kushuhudia,


Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,


Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!


Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atakaribia mbele ya Mungu kwa kuhakikisha kwamba yeye hakuiba mali ya mwenzake.


Mutu akiwakulishia nyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachilia nyama wake kula katika shamba la mutu mwingine, atalipa hasara ile kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.


Mwizi akikamatwa yuko anavunja nyumba, naye akipigwa na kufa, aliyemwua hana kosa la mauaji.


Kama akirudisha rehani na kurudisha kitu alichoiba, akifuata masharti yanayoleta uzima bila kutenda uovu, mutu huyo hakika ataishi. Hatakufa.


Kila siku Haruni anapoingia kwa kutayarisha taa zinazokuwa pale, atafukiza ubani wenye harufu nzuri juu ya mazabahu hiyo.


Sisi wote, watu wote, makuhani na Walawi tutapiga kura kila mwaka kwa kuchagua ukoo utakaoleta kuni za kuteketeza sadaka juu ya mazabahu ya Yawe, Mungu wetu, kufuatana na Sheria.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite