Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kama mutu yeyote akitakiwa kutoa ushuhuda kwenye baraza juu ya jambo aliloona au kusikia naye akikataa kusema kitu, basi, huo ni uovu na atabeba azabu ya zambi ile.

Gade chapit la Kopi




Walawi 5:1
22 Referans Kwoze  

Mutu yeyote akitenda zambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Yawe, yeye ana kosa, na atalipa azabu ya kosa lake.


Anayeshirikiana na mwizi anajizuru mwenyewe; anasikia laana ikitolewa bila kusema neno.


Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.


Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani inakuliwa kwa siku ya tatu, mutu aliyeitoa hatakubaliwa, wala hiyo sadaka haitapokelewa kwa faida yake. Nyama hiyo ni chukizo na mutu atakayeikula atabeba lazima ya uovu wake.


Mujue kwamba uzima wa kila mutu ni katika mikono yangu, ikiwa uzima wa muzazi na uzima wa mutoto. Yeyote anayetenda zambi, ndiye atakayekufa.


“Mutu akimukosea mwenzake, naye akiletwa apate kuapa mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii, naye akiapa,


Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.


Kama mwanaume yeyote akimwoa dada yake, binti ya baba yake au mama yake na binti huyo akakubaliana na mwanaume huyo ambaye ni kaka yake, na kulala naye, hilo ni chukizo. Wanapaswa kutengwa na watu wao maana wamefanya jambo la haya. Huyo mwanaume atabeba lazima ya uovu wake, maana amelala na dada yake.


Lakini kama hafui nguo zake na kuoga, mutu huyu atabeba lazima ya uovu wake.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Atakayetenda zambi huyo ndiye atakayekufa. Mutoto hatabeba uovu wa baba yake, wala baba hatabeba uovu wa mutoto wake. Uhaki wa mutu wa haki itamufalia yeye mwenyewe: na uovu wa mwovu ataubeba yeye mwenyewe.


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


maana nikipata mali mengi nitakusahau; nikisema: “Yawe ni nani?” Au nikiwa masikini nitaiba, na kuzaraulisha jina lako ee Mungu wangu.


Hakuna uzima katika mwili wangu, kwa sababu umenikasirikia. Hakuna afya hata katika mifupa yangu, kwa sababu ya zambi yangu.


Lakini mufalme akamwambia: “Nitakuapisha mara ngapi kwamba kila mara unaposema nami kwa jina la Yawe, unapaswa kuniambia ukweli?”


Lakini mufalme akamwambia: “Nitakuapisha mara ngapi kwamba unaposema nami kwa jina la Yawe, unapaswa kuniambia ukweli mutupu?”


Siku moja akamwambia mama yake: “Vile vikoroti vya feza elfu moja na mia moja ulivyoibiwa, nawe ukamulaani aliyekuiba nami nikiwa ninasikia, mimi niko navyo. Mimi ndiye niliyevibeba.” Mama yake akasema: “Mwana wangu ubarikiwe na Yawe.”


Kama mutu yeyote akikosa kwa kutenda zambi bila kujua juu ya kutokutoa vitu vitakatifu Yawe anavyotolewa, atamuletea kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake. Wewe utapima bei yake kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya kosa.


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Kama mutu akitenda zambi bila kukusudia, akifanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe, atafanya hivi:


Lakini kama aliibiwa kwake, anapaswa kumulipa mwenye naye.


Maana, inchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya laana, inchi inaomboleza, na mashamba ya kulishia nyama yamekauka. Mienendo ya watu ni miovu, wanapoteza nguvu kwa ajili ya mambo yasiokuwa ya haki.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite