Walawi 4:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200221 Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii. Gade chapit la |
Kisha, watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakamutolea Mungu wa Israeli sadaka zao za kuteketezwa kwa moto. Wakatoa ngombe dume kumi na wawili kwa ajili ya Israeli yote, kondoo dume makumi kenda na sita na wana-kondoo makumi saba na saba; vilevile walitoa mbuzi kumi na wawili kama sadaka ya kusamehewa zambi. Nyama wote hawa walitolewa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.
basi, ikiwa kosa hilo limefanyika bila kukusudia, bila Waisraeli wote pamoja kujua, watatoa mwana-ngombe dume mumoja kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe, pamoja na sadaka yake ya vyakula na ya kinywaji kufuatana na maagizo yake. Vilevile watu watatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi.