Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.
Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.
Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii.