Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 27:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu akifanya kiapo cha kumutolea Yawe mwanadamu, mutu huyu anaweza kuondoa kiapo chake kwa kulipa kipimo cha feza kinachokadiriwa kama hivi:

Gade chapit la Kopi




Walawi 27:2
14 Referans Kwoze  

Uwape Waisraeli maagizo haya: Ikiwa mwanaume au mwanamuke atafanya kiapo kuwa munaziri, ni kusema kujitenga kwa ajili ya Yawe,


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Nyuma ya miezi miwili akarudi kwao. Kisha baba yake akamutendea kulingana na kiapo chake. Binti huyo hakukuwa amemujua mwanaume yeyote. Basi, tangu wakati ule kukakuwa desturi hii katika Israeli:


Mutu akiahidi mbele ya Yawe au akifanya kiapo, anapaswa kutimiza ahadi yake. Anapaswa kushika yale yote aliyotamka kwa kinywa chake.


Hapo, Waisraeli wakamwekea Yawe kiapo wakisema: Kama ukiwatia watu hawa katika mikono yetu, basi tutaangamiza kabisa miji yao.


Yawe akamwambia Musa:


Ukuwe mwangalifu kutimiza kiapo ulichosema kwa mudomo wako, maana ulimwahidi Yawe, Mungu wako, kwa mapenzi yako.


Yoasi akaita makuhani na kuwaamuru, akisema: “Kila kuhani apokee feza yote inayotolewa katika nyumba ya Yawe: ni kusema malipo ya kodi za hekalu na matoleo ya mapenzi. Azipokee kutoka kwa yeyote anayemufahamu kwa kutengeneza nyumba popote panapohitajika.”


Ukimutolea Mungu ahadi, usikawie kuitimiza. Mungu hapendezwi na wapumbafu. Timiza kile ulichoahidi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite