Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 26:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nitawapa amani katika inchi hata muweze kulala bila kuogopeshwa na chochote. Nitaondoa nyama wakali katika inchi na inchi yenu haitapatwa na vita.

Gade chapit la Kopi




Walawi 26:6
43 Referans Kwoze  

humo hamutakuwa simba, nyama yeyote mukali hatapitia humo, hao hawatapatikana humo. Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Analeta amani katika eneo lako; anakushibisha kwa ngano safi kabisa.


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Nyumba mupya itakuwa yenye utukufu zaidi kuliko ile ya kwanza. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo! Kutoka hapa nitawapa watu wangu fanaka. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Yawe awape watu wake nguvu! Yawe awabariki watu wake kwa amani!


Tena nitatuma nyama wa pori katika inchi hiyo na kuwanyanganya watoto wao na kuifanya inchi hiyo kuwa ukiwa, hata hakuna mutu yeyote atakayeweza kupita katika inchi ile kwa sababu ya nyama wakali.


Utalala bila kuogopeshwa na mutu; watu wengi watakuomba musaada.


Sitawaondoa watu wale katika mwaka mumoja, inchi isibakie tupu na nyama wa pori wasiongezeke sana na kuwazidia nguvu.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Tena nitaleta vita juu ya inchi ile na kuamuru waiangamize na kuua watu na nyama wanaokuwa ndani yake.


Nitakutumia njaa na nyama wakali ambao wataua watoto wako; magonjwa makali, mauaji, na vita itakuja kukuangamiza. Ni mimi, Yawe, ninayesema hivyo.


Utuonyeshe wema wako, ee Yawe, utujalie wokovu wako.


Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.


Hata hivyo, utapata mwana ambaye atatawala kwa amani kwa sababu nitamupa amani na waadui zake wote wa jirani. Jina lake litakuwa Solomono, kwa maana katika siku za utawala wake, atailetea inchi ya Israeli amani na utulivu.


Elisha aligeuka, akawaangalia na kuwalaani kwa jina la Yawe. Dubu wawili wakatoka katika pori, wakawararua vijana makumi ine na wawili kati yao.


Sasa kufuatana na vile tumekwisha kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani, kunakuwa sasa amani kati yetu na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Ndiyo maana mutu ataweza kusema hivi: Niliamuka nikatambua kwamba usingizi wangu ulinifalia sana.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Ninakulilia kwa sauti, ee Mungu, nawe unanisikiliza kutoka kwenye mulima wako mutakatifu.


Yatakuongoza katika njia yako, yatakulinda wakati unapolala, yatakushauria unapoamuka.


Unapolala, hautakuwa na hofu, utapata usingizi muzuri.


Nawe utapatana na mawe ya shamba, na nyama wakali watakuwa na amani nawe.


Nitaleta nyama wakali kati yenu ambao watawanyanganya watoto wenu na kula mifugo yenu na kupunguza hesabu yenu hata njia zenu zigeuke kama jangwa.


Mutafukuza waadui zenu na kuwaua kwa upanga.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Kwa hiyo, mutafuata masharti yangu na kutimiza maagizo yangu, kusudi mupate kuendelea kuishi kwa usalama katika inchi.


Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.


Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


Ngombe wetu wakuwe na afya na nguvu, kusitokwe mimba wala kukosa kuibeba. Kusikuwe tena kilio katika mitaa yetu.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite