Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 26:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 wakitambua kwa nini nilipingana nao na kuwapeleka katika inchi ya waadui zao, kama kweli moyo wao mugumu ukinyenyekea na kutubu uovu wao,

Gade chapit la Kopi




Walawi 26:41
39 Referans Kwoze  

Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


“Ninyi watu wagumu! Ninyi wenye roho ya kipagani na masikio yanayofungana! Siku zote munapingana na Roho Mutakatifu sawa vile babu zenu walivyofanya!


Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Kwa hiyo kasirani ikakuwa juu yake, juu ya inchi ya Yuda na juu ya Yerusalema. Kisha Hezekia akanyenyekea akaacha kuwa na moyo uliojaa majivuno, yeye na wakaaji wa Yerusalema wakajinyenyekeza; kwa hiyo kasirani ya Yawe haikuwafikia wakati wa utawala wa Hezekia.


“Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele yangu? Basi, kwa sababu amejinyenyekeza, sitaleta yale maangamizi atakapokuwa angali anaishi, lakini nyakati za utawala wa mwana wake nitaiangamiza jamaa ya Ahabu.”


Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.


Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.


Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.


Nitaongea na nani nipate kumwonya, kusudi wapate kunisikia? Angalia, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Maneno ya Yawe, yamegeuka kwao jambo la kuchekelea. Hawalifurahii hata kidogo.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Na yeyote anayejiinua, atashushwa, lakini anayejishusha, atainuliwa.


Sasa, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hakuna mutu yeyote wa taifa la kigeni, asiyetahiriwa au asiyenitii mimi atakayeruhusiwa kuingia katika hekalu langu; hata wageni wanaoishi kati ya Waisraeli, hawataruhusiwa.


Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.


Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.


Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.


Alipojinyenyekeza, Yawe akaacha kumukasirikia na hakumwangamiza kabisa. Zaidi ya hayo, hali ya inchi ya Yuda ilikuwa nzuri.


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


basi, nami nitapingana nanyi na kuwaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


basi nami nitapingana nanyi kwa hasira kali, na kuwaazibu mimi mwenyewe mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Anapaswa kutubu zambi yake aliyotenda; na atatoa malipo kamilifu kwa kosa lake, akiongeza asilimia makumi mbili ya malipo hayo; atatoa malipo hayo kwa yule aliyemukosea.


Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.


Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”


Mienendo na matendo yao vitakuhakikishia kwamba hasara niliyouletea muji huo sikuileta bila sababu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite