Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 26:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 nitawanyeshea mvua kwa wakati unaofaa, inchi ipate kuzaa mavuno kwa wingi, nayo miti ya mashamba matunda yake.

Gade chapit la Kopi




Walawi 26:4
31 Referans Kwoze  

Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


Watu wakusifu, ee Mungu, watu wote wakusifu!


Nitayazidisha matunda ya miti na mazao ya mashamba kusudi musizarauliwe tena kwa ajili ya njaa kati ya mataifa.


Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.


Ananyeshea inchi mvua, anapeleka maji katika mashamba.


Yawe atawafungulia hazina yake nzuri kutoka mbinguni na kunyesha mvua katika inchi kwa wakati wake, na kubariki kazi zenu. Mutakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa.


yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.


Basi! Mimi nitabariki inchi katika mwaka wa sita nayo itawapa mazao ya kuwatoshelea kwa miaka mitatu.


Ingawa vile hakuacha kujijulisha kwa njia ya kutenda mema. Anawanyeshea mvua toka mbingu, anawapa mavuno kwa wakati wake, anawapa chakula na kuwajaza na furaha.”


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Uaminifu utachipuka katika inchi; haki utashuka toka mbinguni.


dunia ilitetemeka, mbingu zilitiririsha mvua; mbele yako, Mungu wa Sinai, mbele yako, Mungu wa Israeli!


Nao wako na uwezo wa kufunga mbingu kusudi mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Wako vilevile na uwezo wa kugeuza maji kuwa damu, na uwezo wa kuleta mapigo ya kila namna kila wakati wanapotaka.


Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha.


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Toka juu angani, unainyeshea milima mvua, nayo dunia unaishibisha kwa baraka yako.


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.


“Basi, mukitii amri zangu ninazowapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kumutumikia kwa moyo wenu wote na kwa roho yenu yote,


Inchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki.


Kweli, Yawe atatuletea baraka, na inchi yetu itatoa mazao yake mengi.


Musiogope, enyi nyama, malisho katika mbuga yamekuwa mazuri, miti inazaa matunda yake, mizabibu na mitini zinazaa kwa wingi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite