Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 26:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Nitaweka makao yangu kati yenu, wala sitawaachilia.

Gade chapit la Kopi




Walawi 26:11
27 Referans Kwoze  

Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, kusudi niweze kukaa kati yao.


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao.


Katika kuungana pamoja na Kristo, ninyi vilevile munaunganishwa pamoja na wengine wote kuwa makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.


Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.


Mungu anajulikana katika Yuda; jina lake ni kubwa katika Israeli.


Musifuate desturi za taifa ninalofukuza mbele yenu. Maana waliyafanya hayo yote, nami nikawachukia sana.


“Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea?


Hakika, nimekujengea nyumba ya kukaa, pahali pa makao yako ya milele.”


Basi, ikiwa inchi yenu muliorizi ni chafu, mukuje katika inchi ya Yawe ambako hema yake iko na kujitwalia sehemu kule pamoja nasi; lakini tu musimwasi Yawe na kutufanya sisi wote waasi kwa kujijengea ninyi wenyewe mazabahu isiyokuwa ya Yawe, Mungu wetu.


Yawe amechukia mazabahu yake na hekalu lake amelikataa. Amewaachilia waadui wazibomoe kuta za nyumba zake katika muji. Wakapiga kelele ndani ya nyumba ya Yawe kama kelele za wakati wa sikukuu.


Usitutupe, kwa ajili ya heshima ya jina lako; usikizarau kiti chako cha kifalme chenye utukufu. Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.


Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


Mungu alipoona hayo, akawaka hasira; akamukataa Israeli kabisa.


Ndiyo maana wanasimama mbele ya kiti cha kifalme cha Mungu, nao wanamutumikia muchana na usiku katika hekalu lake. Na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme atawalinda katika hema yake.


Hapo ndipo watakapotambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, niliyewaleta kutoka katika inchi ya Misri, kusudi niishi kati yao. Mimi ni Yawe, Mungu wao.


kama mukizarau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mukiacha kutii amri zangu zote na kuvunja agano langu,


Wakati watakapokuwa inje ya inchi yao, inchi hiyo itafurahia Sabato zake hapo itakapokuwa katika hali ya ukiwa. Wakati huo wao watatubu uovu wao wa kuzarau maagizo yangu na kuchukia masharti yangu.


Lakini, kwa hayo yote, wanapokuwa katika inchi ya waadui zao, mimi sitawatupa wala kuwachukia hata kuwaangamiza kabisa na kuvunja agano langu.


Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akayaambia makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase: “Leo tumejua kwamba Yawe yuko kati yenu maana hamukumufanyia Mungu uasi. Sasa mumewaokoa Waisraeli wasiazibiwe na Yawe.”


Kila pahali ambako nimekwenda na Waisraeli wote, sikumwuliza mwamuzi yeyote wa Israeli ambaye nilimwamuru awachunge watu wa Israeli: ‘Kwa nini haujanijengea nyumba ya mierezi?’


Mimi nitakaa kati ya wazao wa Waisraeli, na sitawaacha hata kidogo watu wangu, Waisraeli.”


Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite