Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 23:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akamwambia Musa:

Gade chapit la Kopi




Walawi 23:1
13 Referans Kwoze  

Ni mimi niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu. Mimi ni Yawe.


Uwaambie Waisraeli hivi: Katika sikukuu zangu mimi Yawe ambazo zimepangwa mutakuwa na mukutano mutakatifu. Sikukuu ambazo nimepanga ni hizi:


mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,


Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.


Musa akawatangazia Waisraeli sikukuu za Yawe zilizopangwa.


na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.


Nyumba ninayokusudia kujenga itakuwa kubwa sana, maana Mungu wetu ni mukubwa zaidi ya miungu yote.


Alitoa sadaka zile kadiri ilivyotakiwa na amri ya Musa kila siku takatifu, ni kusema siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, na sikukuu tatu za kila mwaka – sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, sikukuu ya majuma na sikukuu ya vibanda.


Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.


Kukikuwa magombano wataamua kadiri ya maamuzi yangu. Katika sikukuu zote watafuata sheria zangu na maamuzi yangu, na kuzitakasa Sabato zangu.


Wakati wa siku za sikukuu na siku zilizopangwa, sadaka za unga zitakuwa litre kumi na saba zikiandamana na kila ngombe dume au kondoo dume, na chochote ambacho anayeabudu anaweza kutoa kwa kila mwana-kondoo. Kwa kila sadaka ya unga atatoa litre tatu za mafuta.


Kwa nini munashugulika na kutimiza desturi zenu za siku, miezi, nyakati na za miaka?


Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite