Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akamwambia Musa: Uwaambie makuhani, wana wa Haruni, kwamba kusikuwe mutu yeyote kati yao atakayejichafua kwa kugusa maiti ya watu wa jamaa yake,

Gade chapit la Kopi




Walawi 21:1
12 Referans Kwoze  

Hawatasogelea maiti kusudi wasijichafue. Lakini wataweza kujichafua kwa kusogelea maiti ya baba au mama au mutoto wa kike au wa kiume au dada asiyeolewa.


Na hii ndiyo sheria ya kufuatwa kama mutu akikufia ndani ya hema: Kila mutu atakayeingia ndani ya hema hilo, au aliyekuwa ndani ya hema hilo, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Asikaribie maiti wala kujichafua kwa maiti hata kama ni ya baba yake au ya mama yake.


Musijitie chanjo juu ya mwili wenu kwa ajili ya kuomboleza au kujikatakata chanjo yoyote juu ya mwili. Mimi ni Yawe.


Hivyo mutajua kwamba nimewapa amri hii kusudi agano langu na ukoo wa Lawi likuwe la kudumu.


Yawe wa majeshi anawaambia makuhani: Sasa enyi makuhani, ninawaamuru hivi:


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


Mutu yeyote akigusa mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida inje ya nyumba, au akigusa mufupa wa mutu au kaburi, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Uwaamuru Waisraeli wamutoe inje ya kambi kila mutu mwenye ukoma, kila mutu anayetokwa usaha, na kila anayekuwa muchafu kwa kugusa maiti.


Siku zote atakazokuwa amejitakasa kwa Yawe, mutu huyo asikaribie maiti,


Mutu akigusa maiti ya mutu yeyote, atakuwa muchafu kwa siku saba.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite