Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 19:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kama sehemu ya nyama yake ikikuliwa siku ya tatu, tendo hilo ni chukizo na sadaka hiyo haitakubaliwa.

Gade chapit la Kopi




Walawi 19:7
9 Referans Kwoze  

Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Wanaikaa katika makaburi na kupitisha usiku ndani ya mashimo. Wanakula nyama ya nguruwe na kuweka muchuzi wa nyama wachafu ndani ya sahani zao.


Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.


Wala usipokee kutoka kwa wageni nyama wa namna hiyo na kunitolea mimi Mungu wako kama chakula. Nyama hao wana kilema kwa vile wamekatwa na hawatakubaliwa kwa faida yenu.


Ngombe dume au mwana-kondoo anayekuwa na kiungo kimoja kirefu au kifupi kuliko kawaida wanaweza kumutoa sadaka ya mapenzi. Lakini huyo usimutoe kuwa sadaka ya kutimiza kiapo.


Sadaka hiyo inapaswa kuliwa siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki mpaka kwa siku ya tatu kinapaswa kuteketezwa kwa moto.


Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite