Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kuhani atamuchunguza tena mutu yule siku ya saba. Kama kulingana na uchunguzi wake, ile sehemu ya ugonjwa imefifia na ugonjwa haujaenea, basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa safi, huo ni upele tu. Mutu huyo atafua nguo zake, naye atakuwa safi.

Gade chapit la Kopi




Walawi 13:6
23 Referans Kwoze  

Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.


Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.


Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Mumupokee yule anayekuwa zaifu katika imani pasipo kubishana naye juu ya mawazo yake.


Hatavunja tete lililokunjama, hatazimisha utambi unaotoa moshi; ataimarisha sheria yangu kwa uaminifu.


Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.


Nani anayesubutu kusema: “Nimetakasa moyo wangu; mimi nimetakasika na zambi yangu?”


Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.


usikilize kutoka mbinguni wanapokuomba na kukusihi. Uwapatie ushindi katika vita.


tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,


Lakini ninyi mumekosa uaminifu kwake, ninyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu, ninyi ni kizazi kiovu na kipotovu.


Ikiwa mutu yeyote atakuwa na kivimba au upele au chunuku juu ya mwili wake, ikionekana kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Haruni au mumoja wa wana wake anayekuwa kuhani.


Mutu yeyote akikula nyama ya muzoga huo atafua nguo yake na atakuwa muchafu mpaka magaribi. Na yeyote atakayebeba muzoga huo, atafua nguo zake, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Mutu yeyote anayebeba muzoga atakuwa muchafu mpaka magaribi, naye atasafisha nguo zake. Hao ni wachafu kwenu.


Siku ya saba, kuhani atamwangalia tena mutu yule, na ikiwa, kulingana na uchunguzi wa kuhani, ugonjwa huo haujaenea kwenye ngozi yake, basi, kuhani atamutenga mutu yule kwa siku zingine saba.


Lakini taka lile likienea kwenye ngozi, nyuma ya mutu yule kujionyesha kwa kuhani kwa ajili ya kutakaswa kwake, basi, atakuja tena kwa kuhani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite