Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Ikiwa mutu yeyote atakuwa na kivimba au upele au chunuku juu ya mwili wake, ikionekana kwamba ni ukoma, basi, ataletwa kwa kuhani Haruni au mumoja wa wana wake anayekuwa kuhani.

Gade chapit la Kopi




Walawi 13:2
23 Referans Kwoze  

“Kama mutu akishikwa na ukoma munapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama vile nilivyowaamuru ndivyo mutakavyofuata kwa uangalifu.


kivimba, jipu au chunuku,


Kuhani atakwenda kumwangalia yule mutu inje ya kambi. Ikiwa ukoma huo umepona,


Yesu alipowaona, akawaambia: “Mwende kwa makuhani kusudi wapate kuwachunguza.” Nao walipokuwa katika njia kwenda kule, wakaponyeshwa.


Yesu akamwamuru hivi: “Usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


“Angalisho, usimwambie mutu hata neno moja juu ya hii. Lakini kwenda kwa kuhani na kumwonyesha jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa wote kwamba umetakaswa.”


Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Basi, mimi Yawe nitawaazibu; nitawanyoa nywele hao wanawake wa Sayuni, na kuwavua nguo za kufunika uchi wao.


Tokea kwenye muguu mpaka kwenye kichwa hakuna chenye kuwa kizima; ni machubuko, alama za mapigo na vidonda vinavyovuja damu, vilivyokosa kusafishwa, kufungwa wala kutulizwa kwa mafuta.


Kwa hiyo ukoma wa Namani utakushika wewe, na wazao wako milele.” Basi, Gehazi aliondoka akiwa ameshikwa na ukoma, na ngozi yake ilikuwa nyeupe kama teluji.


Namani, jemadari wa waaskari wa mufalme wa Aramu, alikuwa mutu mukubwa aliyeheshimiwa sana na bwana wake, maana kwa njia yake Yawe aliiletea inchi ya Waaramu ushindi. Alikuwa askari hodari, lakini alikuwa na ugonjwa wa ukoma.


Lazima ya mauaji hayo yakuwe juu ya kichwa cha Yoabu na jamaa yote ya baba yake! Jamaa ya Yoabu isikose mutu mwenye ugonjwa wa kisonono siku zote, au ugonjwa wa ukoma, au anayetembelea kwa miti au kuuawa kwa upanga, au mwenye kukosa chakula!”


Yawe atawapiga kwa majipu yaliyowapata Wamisri, atawapa vidonda, upele na kuwashwa ambavyo hamuwezi kuponywa.


Wingu lilipoondoka juu ya hema la mukutano, Miriamu akaonekana yuko na ukoma, mweupe kama teluji. Haruni alipogeuka na kumwangalia Miriamu, akashangaa kuona kwamba ameshikwa na ukoma.


basi, mwenye nyumba hiyo anapaswa kumwambia kuhani kwamba namna ya taka la ukoma imeonekana katika nyumba yake.


Usimufanye Miriamu akuwe kama mutu aliyezaliwa mufu, ambaye karibu nusu ya mwili wake imeozeshwa.


Yawe akawaambia Musa na Haruni:


Kuhani atachunguza pahali panapokuwa ugonjwa na ikiwa nywele za pahali pale zimebadilika kuwa nyeupe na ugonjwa wenyewe ukionekana kuwa uko ndani zaidi ya ngozi ya mwili wake, basi, huo ni ukoma. Kuhani akimaliza kumuchunguza, hivyo atatangaza kwamba mutu yule ni muchafu.


Kuhani atamwangalia tena, na kama ule upele umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa muchafu, huo ni ukoma.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite