Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.
Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.
Nilitahiriwa nilipokuwa na umri wa siku nane. Mimi ni Mwisraeli, wa kabila la Benjamina, Mwebrania wa asili kabisa. Kuelekea mambo ya Sheria ya Kiyuda, nilikuwa Mufarisayo,
Mambo ninayotaka kusema ni haya: Mungu amekwisha kufanya agano kwa njia ya haki. Nayo Sheria iliyotokea miaka mia ine makumi tatu nyuma yake haiwezi kulivunja au kugeuza ile ahadi ya Mungu.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.
Watu wamoja walishuka toka Yudea kwenda Antiokia, nao wakaanza kuwafundisha wandugu waamini kwamba hawawezi kuokoka ikiwa hawatahiriwi sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ya Musa.
Kisha mama wa mutoto ataendelea kuwa muchafu kwa muda wa siku makumi tatu na tatu. Wakati huo, asiguse chochote kilichotakaswa wala kuingia Pahali Patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia.