Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.

Gade chapit la Kopi




Walawi 10:9
17 Referans Kwoze  

kwa maana atahesabiwa kuwa mutu mukubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kinywaji kikali, na atajazwa na Roho Mutakatifu tangu kuzaliwa kwake.


Hapaswi kuwa mulevi wala mupiganaji, lakini akuwe mupole mwenye kupenda amani, wala asikuwe mutu wa kupenda feza.


Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Kuhani yeyote asikunywe divai anapoingia katika kiwanja cha ndani.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;


basi, asikunywe divai au kileo, asikunywe siki ya divai au ya namna nyingine, asikunywe maji ya zabibu wala kula zabibu zilizoiva au kavu.


Kwa ajili ya maumivu ya tumbo lako na uzaifu wa mwili wako wa kila mara, tangu sasa usikunywe maji tu, lakini utumie divai kidogo.


Uasherati, divai mupya na ya zamani vinaondoa maarifa.


Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.


Halafu kuhani atavitikisa vitu hivyo kama sadaka ya kutikisa mbele ya Yawe; vyote hivi ni sehemu takatifu kwa kuhani, pamoja na kilali kilichotikiswa na paja lililotolewa kama sadaka. Nyuma ya hayo yote, munaziri anaweza kunywa divai.


Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.


Yawe akaongea na Haruni, akasema:


Hiyo itakuwa ndani ya hema la mukutano inje ya pazia lile mbele ya Sanduku la Agano na Haruni na wana wake wataitunza mbele yangu tangu magaribi mpaka asubui. Sharti hili lifuatwe siku zote na Waisraeli wote, kizazi kwa kizazi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite