Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 10:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, Musa akachunguza kwa uangalifu juu ya mbuzi mumoja aliyetolewa sadaka kwa ajili ya zambi, akatambua kwamba alikwisha kuteketezwa kwa moto. Hivyo akawakasirikia sana Eleazari na Itamari, wana wa Haruni waliobakia, akawauliza:

Gade chapit la Kopi




Walawi 10:16
12 Referans Kwoze  

Uwaambie Waisraeli watwae beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi, na mwana-ngombe mumoja na mwana-kondoo mumoja wote wa umri wa mwaka mumoja na wasiokuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,


Kisha, Haruni akaleta mbele sadaka ya watu. Akatwaa mbuzi wa sadaka ya watu kwa ajili ya zambi, akamuchinja na kumutoa sadaka kwa ajili ya zambi, kama vile alivyofanya kwa yule wa kwanza.


Kama mukikasirika, musianguke katika zambi, kasirani yenu isidumu muchana kutwa,


Yesu alipoona vile, akakasirika na kuwaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)


Yawe akamwambia Musa:


mwana wa Abisua mwana wa Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni, Kuhani Mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite