Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Walawi 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Musa akamwambia Haruni na wana wake waliobakia, Eleazari na Itamari: Mutwae ile sehemu ya sadaka ya vyakula iliyobakia kutoka sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Muikule karibu na mazabahu bila kutiwa chachu kwa sababu ni takatifu kabisa.

Gade chapit la Kopi




Walawi 10:12
14 Referans Kwoze  

Mutu huyo anaweza kula mukate wa Mungu wake, vitu vitakatifu na vile vitakatifu kabisa.


Watakula sadaka ya vyakula, sadaka ya kusamehewa zambi, na sadaka ya malipo ya kosa. Kila kitu katika Israeli kilichotakaswa kwa Mungu kitakuwa chao.


Sadaka yoyote ya ngano iliyopikwa juu ya mafika katika chungu au katika kikaango itakuwa mali ya kuhani anayeitolea.


mikate isiyotiwa chachu, maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopondwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyotiwa chachu, lakini iliyopakwa mafuta. Vyote hivi vikuwe vimetengenezwa kwa unga laini wa ngano.


Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.


Mutaikula katika Pahali Patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazao wako kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hivi ndivyo nilivyoamuriwa.


Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni: Nadabu, muzaliwa wake wa kwanza, Abihu, Eleazari na Itamari.


Watakula vitu hivyo vilivyotumika kwa utakaso na kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho, lakini mutu mwingine asiruhusiwe kuvikula maana ni vitakatifu.


Haruni na wazao wake peke yao ndio wanaoruhusiwa kula mikate hiyo maana ni mitakatifu kabisa kwa sababu ni sehemu ya sadaka ninazotolewa mimi Yawe kwa moto. Hiyo ni haki yao milele.


Kore mwana wa Imuna, Mulawi, aliyekuwa mulinzi wa Mulango wa Mashariki wa hekalu, akasimamia matoleo yote ya mapenzi kwa Mungu; na kugawanya matoleo kwa ajili ya Yawe na sadaka zinazokuwa takatifu kabisa.


mwana wa Abisua mwana wa Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni, Kuhani Mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite