Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mushike mambo yote muliyojifunza na kupokea toka kwangu, nayo yote muliyosikia na kuona kwangu. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 4:9
36 Referans Kwoze  

Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.


Wandugu zangu, mufuate mufano wangu, muwaangalie vizuri wale wanaofuata mwenendo muliouona kwetu.


Kwa hiyo wandugu zangu, kufuatana na vile mulivyochaguliwa na kuitwa na Mungu, mufanye nguvu zaidi kwa kukamilika katika njia ile. Mukitenda mambo yale hamutaanguka hata kidogo.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Na amani ya Mungu inayopita ufahamu wa mutu yeyote, italinda mioyo yenu na nia zenu salama katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


“Sababu gani munaniita ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamufanyi yale ninayowaamuru?


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Bwana anatupatia tumaini kwa ajili yenu kwamba munafanya na mutaendelea kufanya yale tunayowaagiza.


Ninyi mumefuata mufano wetu na mufano wa Bwana, kwa kuwa ingawa muliteswa sana, mulipokea neno la Mungu kwa furaha inayotoka kwa Roho Mutakatifu.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Basi Mungu anayeleta amani akuwe pamoja nanyi wote. Amina!


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


Lakini Yesu akawajibu: “Mama yangu na wandugu zangu ni wale wanaosikia neno la Mungu na kulishika.”


Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Bwana akulinde. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.


kwa maana Mungu hataki sisi tuishi katika fujo, lakini katika amani. Sawa vile inavyokuwa desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu,


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Basi ninawasihi, mufuate mufano wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite