Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 4:8
67 Referans Kwoze  

Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Na wewe unapaswa kuwa mufano katika matendo mema, ukionyesha ukweli na heshima katika mafundisho yako.


Kwa maana tunataka kufanya mema, si mbele ya Bwana tu, lakini mbele ya watu vilevile.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Muzidi kutuombea. Tuna uhakika kwamba tuko na zamiri safi, kwa maana tunataka kuwa na mwenendo mwema katika mambo yote.


Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.


kwa maana matunda ya mwangaza ni wema wa kila namna, haki na ukweli.


Lakini inafaa akuwe mwenye kupenda kukaribisha wageni, mwenye kupenda mema, mukadirifu, mwenye haki, mutakatifu na mutaratibu.


Basi, kila mutu anayekuwa na tumaini hili katika Kristo anajisafisha mwenyewe kama vile Kristo anavyokuwa safi.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Inafaa watu wetu vilevile wajifunze kuzidi kutenda mema kusudi wapate kutoa musaada kwa ajili ya mahitaji ya kweli. Na hivi maisha yao yatakuwa yenye mafaa.


Tukuwe na mwenendo muzuri unaostahili wakati wa muchana, tukijilinda na ulafi na ulevi, uasherati na uzinzi, magombano na wivu.


Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


Watoto wangu, upendo wetu usikuwe wa masemi tu; lakini unapaswa kuwa upendo wa kweli na unaoonekana kwa matendo.


Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.


Nasi tunaomba Mungu kusudi musifanye jambo lolote baya, nasi hatutaki kuonyesha kwamba tumeshinda. Lakini tunataka mutende mema hata ikionekana kuwa sisi tunashindwa.


Mukuwe na mwenendo wa hekima mbele ya watu wanaokuwa wa inje ya kanisa, mukitumia vema kila wakati munaoupata.


Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.


Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Kwa maana wanaofanya mema hawaogopi watawala, lakini wale wanaofanya mabaya. Unataka kuishi bila kumwogopa mwenye mamlaka? Basi fanya mema naye atakusifu,


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, mufurahi kwa ajili ya kuungana kwenu na Bwana. Hainiuzi kitu kuwaandikia tena maneno yale yale niliyowaandikia mbele. Hayo yote ni kwa ajili ya kuwakingia hatari.


Lakini Muyuda wa kweli ni yule anayekuwa Muyuda kwa ndani, nako kutahiriwa kwa kweli ni kule Roho Mutakatifu anakofanya ndani ya moyo wa mutu, wala si kule kunakofanyika kwa njia ya maandiko ya Sheria. Mutu wa namna hii hapati sifa kutoka kwa watu lakini kutoka kwa Mungu.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Jasho lake linastahili kulipwa. Shuguli zake zinapaswa kuheshimiwa popote.


Inafaa kuombea wafalme na watu wenye mamlaka kusudi tupate kuishi katika ukimya na amani katika kushikamana na ibada na katika mwenendo safi.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Mutafuata yanayokuwa ya haki tu, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi munayopewa na Yawe, Mungu wenu.


Basi, mujiweke tayari: mukijifungia ukweli kama vile mukaba, mukivaa haki kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua,


Hivi mutakuwa na mwenendo wa heshima mbele ya watu wasiokuwa wa Kristo, wala hamutahitaji kusaidiwa na mutu yeyote.


Kwa hivi, muache uongo! Kila mumoja aseme ukweli kwa mwenzake, kwa maana sisi wote ni viungo vya mwili mumoja.


Tunaheshimiwa na kuzarauliwa, tunatukanwa na kusifiwa. Tunahesabiwa kama wenye kusema uongo, ingawa sisi tunasema ukweli,


Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”


Mutu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe, anajitafutia sifa yake mwenyewe. Lakini yeye anayetafuta sifa ya yule aliyemutuma, huyu ni mwenye ukweli wala hana ubaya wowote.


Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;


Herode alimwogopa Yoane, kwa sababu alijua kwamba Yoane ni mwenye haki na mutakatifu. Kwa hivi alimulinda. Alipenda kumusikiliza, ijapokuwa alifazaika sana kila mara alipomusikia.


Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, lakini matumizi ya vipimo vya haki ni furaha kwake.


Sasa binti yangu usifazaike, nitakufanyia lolote utakaloomba kwa sababu kila mutu katika muji huu anajua wema wako.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


“Kule Damasiki kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Anania, mutu aliyeogopa Mungu na mwenye kushika Sheria yetu. Aliheshimiwa sana na Wayuda wote waliokaa kule.


Kinywa chake kinajaa maneno matamu. Yeye wote anapendeza. Basi, hivi ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa, ndivyo rafiki yangu anavyokuwa, enyi wabinti wa Yerusalema.


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


nao wanawake wazee kama mama yako na vijana wanawake kama wadada zako, ukijilinda katika maisha safi.


Kulikuwa mutu mumoja muzaliwa wa Arimatea, katika jimbo la Yuda, jina lake lilikuwa Yosefu. Mutu huyu alikuwa mwema na mwenye haki, naye alikuwa akitazamia Ufalme wa Mungu. Yeye alikuwa mumoja wa washauri wa Baraza Kubwa, lakini hakukubali shauri na matendo ya wenzake.


Anasema: “Wanawake wengi wametenda mambo ya ajabu, lakini wewe umewashinda wote.”


Mizani na vipimo vya kweli ni vya Yawe. Mawe yote ya kupimia katika mufuko ni kazi yake.


Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.


Anapaswa kuwa mutu mwenye kuongoza jamaa yake vizuri na kuadibisha watoto wake kusudi wakuwe wenye utii na wenye heshima kabisa.


Hivi wandugu, muwachague wanaume saba kati yenu wenye ushuhuda muzuri, wenye kujazwa na Roho Mutakatifu na wenye hekima, kusudi tuwaweke kwa kazi hii.


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Muke mwema atapatikana wapi? Bei yake ni kali kuliko ushanga!


Ni kwa sababu ya imani yao babu zetu wameshuhudiwa vizuri na Mungu.


Wanawake wao wanapaswa kuwa na adabu vilevile, wasikuwe wasingiziaji wa uongo, lakini wakuwe wakadirifu na waaminifu katika mambo yote.


Pamoja naye tunamutuma ndugu anayesifiwa na makanisa yote kwa ajili ya kazi yake ya kuhubiri Habari Njema.


Saulo na Yonatani, watu wema na wa kupendeza. Katika maisha na kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, wenye nguvu kuliko simba.


Wapendwa wangu, hii ni sasa barua ya pili ninawaandikia. Katika barua hizi zote mbili nilitaka kuamusha ndani yenu mafikiri safi mupate kukumbuka mambo haya.


“Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu?


Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite