13 Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.
Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.
Mungu atawatia nguvu kwa uwezo wake wenye utukufu, kusudi mupate kuvumilia kila kitu pasipo kuchoka. Basi kwa furaha,
Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.
Ninaomba Mungu, kwa uwingi wa utukufu wake, awajalie nguvu mupate kuwa imara ndani ya roho zenu, kwa njia ya Roho wake.
Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.
Watasema juu yangu: Haki na nguvu viko kwa Yawe peke yake. Wote waliomukasirikia Yawe watakuja kwake na haya.
Ninamushukuru Bwana wetu Kristo Yesu aliyenitia nguvu, kwa sababu alinihesabu kuwa mwaminifu hata akaniweka kwa kazi yake.
Naye Yesu akamujibu: “Kuja.” Halafu Petro akatoka ndani ya chombo, akaanza kutembea juu ya maji kumufikia Yesu.