Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ninajua kuishi katika ukosefu na ninajua kuishi katika utajiri. Nimejizoeza kufurahi fasi zote na katika kila hali: ikiwa hali ya kuwa na vyakula kwa uwingi au ya njaa, ikiwa hali ya utajiri au ya ukosefu.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 4:12
15 Referans Kwoze  

Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.


Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.


Wakati nilipokuwa kwenu, sikumulemea mutu yeyote nilipohitaji kitu fulani, kwa maana wandugu waliotoka Makedonia waliniletea vitu vyote nilivyohitaji. Nilijiangalia vizuri katika mambo yote kusudi nisiwalemee, nami nitaendelea kujiangalia vema.


Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.


Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia:


Mimi niliwatangazia Habari Njema ya Mungu bila kudai mushahara. Nilijinyenyekeza kusudi mupate kutukuzwa. Basi kwa kujinyenyekeza vile, nilifanya kosa?


Kwa sababu wengi wanasema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito; lakini yeye mwenyewe anapokuwa katikati yetu ni muzaifu na namna yake ya kusema ni ya kuzarauliwa.”


Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.


Maana kisha kukuasi, niligeuka toka zambi zangu, na kisha kufundishwa, nilijilaumu, nikapata haya na kufezeheka, maana nilibeba haya za ujana wangu.


Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria; ukawapa mana kuwa chakula chao, na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.


Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite