Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 3:8
53 Referans Kwoze  

Ninaona kwamba mateso ya wakati huu wa sasa hayawezi kupima kulinganishwa na utukufu ambao Mungu atakaoonyesha kwetu waziwazi.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Lakini mambo yote yaliyokuwa ya faida kwangu, sasa kwa ajili ya Kristo, ninayahesabu kama kihombo.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Kitu ninachotaka tu, ni kumujua Kristo na uwezo wa ufufuko wake na kushirikiana naye katika mateso yake, nako kufa kwangu kufanane na kufa kwake.


Kwa uwezo wake, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji katika maisha yetu kusudi tupate kushikamana na kumwabudu yule aliyetuita kushiriki utukufu wa wema wake mwenyewe.


Kwa maana wakati nilipokuwa pamoja nanyi nilikusudia nisijue mambo mengine lakini Yesu Kristo tu na habari ya kufa kwake juu ya musalaba.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile. Na tangu sasa mumemujua, na mumemwona.”


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Hivi, sisi wote tutafikia umoja wa imani yetu na wa kumujua kabisa Mwana wa Mungu; tutapata kukomaa na kufikia kipimo cha utimilifu wa Kristo.


Lakini muzidi kukomaa katika neema na katika kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Asifiwe, sasa na hata milele! Amina.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Kwa maana, mimi sasa niko tayari kutolewa kama sadaka, na wakati wa kufa kwangu umekaribia.


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Watafanya hivi kwa sababu hawakumujua Baba wala mimi.


Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia, watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Basi jiwe lile linahesabiwa kuwa la bei kali kwa wale wanaoamini. Lakini kwa wale wasioamini ni: “Jiwe lililotupiliwa na wajengaji, lakini sasa linakuwa jiwe kubwa la pembe.”


kumufunua Mwana wake kwangu, kusudi nihubiri Habari yake Njema kwa watu wa mataifa mengine. Na pale pale sikuomba shauri kwa mutu yeyote,


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Hasemi maneno haya zaidi sana kwa ajili yetu? Hakika, maneno hayo yaliandikwa kwa ajili yetu. Inafaa yule anayelima na yule anayetwanga watumike wakiwa na tumaini la kupata sehemu yao ya mavuno.


Wale wamalaika wakamwuliza: “Ee mama, kwa sababu gani unalia?” Naye akawajibu: “Kwa sababu wameondoa maiti ya Bwana, nami sijui pahali walipoiweka.”


Kwa ngambo yangu, ikiwa mimi ninafukuza pepo kwa uwezo wa Mungu, hii inaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha kufika kati yenu.


atakayeingia katika inchi hiyo ambayo niliapa kuwapa ikuwe yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.


Namna gani nimepata bahati hii ya kutembelewa na mama ya Bwana wangu?


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


atatupiliwa mbali kama mavi yake. Waliopata kumujua watajiuliza: “Yuko wapi?”


Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mboleo ndani ya shamba katika inchi ya Yezereheli, hata hakuna atakayeweza kumutambua.’ ”


Basi, sasa nitailetea jamaa hii ya Yeroboamu hasara, nitawaua wanaume wote wa jamaa yake katika Israeli, akuwe mutumwa au huru. Watu wa jamaa yake wote nitawateketeza kama vile mutu anavyoteketeza mavi, mpaka yatoweke.


Mbinguni, nani anayeweza kunisaidia isipokuwa wewe? Na katika dunia hamuna ninachokitamani isipokuwa wewe!


wala nguvu za juu, wala nguvu za chini, wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu aliouonyesha kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.


Ninawatakia neema na amani kwa uwingi kufuatana na vile munavyomujua Mungu na Yesu Bwana wetu.


Kwa maana mukiwa na tabia hizi zote kwa uwingi, zitawawezesha kutumika na kuzaa matunda hata mupate kumujua Bwana wetu Yesu Kristo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite