Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Alijinyenyekeza na kutii mpaka kufa, ndiko kufa kwake juu ya musalaba.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 2:8
26 Referans Kwoze  

Hakuna mutu anayeweza kunionodoa uzima, lakini ninajitoa mwenyewe kufa kwa mapenzi yangu. Niko na uwezo wa kujitoa kufa na niko na uwezo wa kuwa tena muzima. Ni vile Baba yangu alivyoniagiza kufanya.”


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Na kama vile kutokana na uasi wa mutu mumoja, watu wengi wamekuwa wenye zambi, ni hivi vilevile kutokana na utii wa mutu mumoja, watu wengi watahesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Alinyenyekezwa na kuhukumiwa bila haki. Hakuna mutu atakayeweza kueleza habari za kizazi chake, maana maisha yake yameondolewa katika dunia.”


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


lakini sherti dunia ijue kama ninamupenda Baba, nami ninafanya kama alivyoniagiza. “Musimame, tutoke hapa.


Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


Akawaacha tena kwa mara ya pili, akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama kikombe hiki cha mateso hakiwezi kupita mbali nami, bila mimi kukikunywa, basi mapenzi yako yafanyike!”


Koo langu limekauka kama kigae; ulimi wangu unanata ndani ya kinywa changu. Wewe umenilaza pembeni ya kaburi.


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Na kule sura ya Yesu ikageuka wazi mbele yao. Uso wake ukangaa kama jua, nazo nguo zake zikametameta kama mwangaza.


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


Naye alipokuwa akiomba, sura yake ikageuka, nazo nguo zake zikageuka nyeupe sana na zenye kumetameta.


Kwa maana katika vita munayofanya kwa kushinda zambi, hamujapigana bado mpaka kufa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite