28 Hivi ninamutuma kwenu kwa haraka kusudi mupate kufurahi wakati mutakapomwona tena na huzuni yangu ipate kupunguka.
Na sasa ninyi vilevile munasikia uchungu, lakini nitawaona tena, nanyi mutafurahi, wala hakuna mutu atakayeweza kuwahuzunisha tena.
Nikikumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona kusudi nipate kujazwa na furaha.
Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.
Walihuzunika zaidi kwa sababu aliwaambia kwamba hawatamwona tena. Wakamusindikiza mpaka kwenye chombo.
Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini, kumbe, Mungu amenijalia hata kuwaona watoto wako!”
Basi mumupokee kwa furaha kubwa sana kwa jina la Bwana. Munapaswa kuwapa watu wa namna hii heshima,