Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 1:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Basi niko na uhakika juu ya jambo hili nami ninajua kwamba nitabaki. Nitakaa pamoja nanyi kwa kuwasaidia kusudi mupate kuendelea na kuwa na furaha katika imani.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 1:25
17 Referans Kwoze  

Nami ninamutumainia Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kuwaona bado kidogo.


Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.


Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.


Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.


“Nilikuwa nikizungukazunguka kati yenu ninyi wote nikitangaza Ufalme wa Mungu. Lakini sasa, ninajua kwamba hakuna hata mumoja atakayeniona tena.


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


Nami ninajua kwamba wakati nitakapokuja kwenu, nitakuja na baraka nyingi sana kutoka kwa Kristo.


Kwa maana sitasubutu kuongeza kitu kingine, isipokuwa tu kile Kristo alichotimiza kwa njia yangu kusudi watu wa mataifa wapate kumutii Mungu. Alifanya vile kwa njia ya yale aliyoniwezesha kusema na kutenda,


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Uwaarifu kwa vitambulisho wale wanaokuheshimu, wapate kuuepuka mushale.


Lakini jambo la lazima zaidi kwa ajili yenu, mimi niendelee kuishi.


Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite