Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Wafilipi 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 kusudi mupate kutambua mambo yanayokuwa bora zaidi. Kwa hivi mutakuwa safi pasipo kosa kwa Siku ile ya kurudia kwa Kristo.

Gade chapit la Kopi




Wafilipi 1:10
43 Referans Kwoze  

Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Unajidai kwamba unajua mapenzi yake na kutambua mambo yanayofaa zaidi kwa sababu umefundishwa na Sheria.


Mujikaze kutambua mambo yanayomupendeza Bwana.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


Ninajua hakika kwamba Mungu aliyeanza kazi hii njema ndani yenu, ataitimiza mpaka siku ile ya kurudi kwa Yesu Kristo.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.


Alitaka hivi kujipatia yeye mwenyewe kanisa tukufu na takatifu, lisilokuwa na taka wala kikunjo wala kilema chochote.


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Kwa maana wale wanaoshugulika na hali ya kimwili ni waadui za Mungu; hawatii sheria ya Mungu wala hawawezi kuitii.


Petro akamujibu: “Hata wote wakianguka, mimi sitaanguka hata kidogo.”


Lakini ninyi munachukia mazuri na kupenda mabaya. Munawachuna ngozi watu wangu, na kunyofoa nyama juu ya mifupa yao.


Sikio linapima maneno, kama vile ulimi unavyoonja chakula.


Sikio halipimi maneno kama vile ulimi unavyoonja chakula?


Si ni Abrahamu mwenyewe ndiye aliyesema kwamba huyu ni dada yake? Tena hata Sara mwenyewe alisema kwamba Abrahamu ni kaka yake! Mimi nimefanya nilivyofanya kwa moyo safi na sina kosa.”


Hawa wanahubiri kwa upendo, kwa maana wanajua kwamba Mungu amenipatia kazi ya kuitetea Habari Njema.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


Lakini tukitangaza ukweli kwa upendo, tutakomaa katika mambo yote na kufikia kuwa kama Kristo, ambaye ni kichwa.


Wandugu, ikiwa mimi ningali ninahubiri ya kama ni lazima kutahiriwa, basi kwa sababu gani ningali ninateswa? Kama ningefanya vile, basi watu hawangechukizwa na mahubiri yangu juu ya musalaba wa Kristo.


Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.


Sisi hatutaki kumukwaza mutu yeyote katika jambo lolote kusudi kazi yetu isizarauliwe.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Basi muangalie, kusudi musiwakwaze Wayuda, wala wasiokuwa Wayuda, wala kanisa la Mungu.


Kwa hiyo chakula kikimwangusha ndugu yangu katika zambi, nitajizuiza kula nyama siku zote kusudi nisimwangushe ndugu yangu.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Ndani ya roho yangu ninapendezwa na Sheria ya Mungu,


Ikiwa kile ninachofanya ndicho nisichotaka, maana yake ninakubali ya kuwa Sheria ni nzuri.


Kwa sababu hii ninajikaza siku zote kuishi maisha safi bila kuhukumiwa na zamiri yangu mbele ya Mungu na mbele ya watu.


Kila mutu anayefanya mabaya anachukia mwangaza, naye anakataa kuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yasionekane wazi.


mukiwatangazia habari inayoleta uzima. Hivi nitapata sababu ya kujivuna Siku ile ya kurudia kwa Kristo kwa maana itakuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite