Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Waefeso 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Na ninyi wabwana muwatendee watumwa wenu hivi vilevile. Muache kuwatisha, mukijua kwamba ninyi na watumwa wenu muko na Bwana mumoja mbinguni, naye hafanyi kitu kwa upendeleo.

Gade chapit la Kopi




Waefeso 6:9
40 Referans Kwoze  

Lakini yule anayefanya mabaya, atalipwa kufuatana na mabaya aliyotenda, kwa sababu Mungu hana upendeleo.


Basi Petro akaanza kuhubiri, akisema: “Sasa ninafahamu kwamba Mungu hana upendeleo,


Kwa maana Mungu hana upendeleo.


Muwatendee wengine sawasawa munavyotaka wawatendee ninyi vilevile.


“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”


Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


Kwa maana mutumwa aliyeitwa kuwa wa Bwana, amepewa uhuru na Bwana. Hivi vilevile mutu mwenye uhuru aliyeitwa na Kristo, ni mutumwa wa Kristo.


Naye atamupiga vikali na atamwazibu sawa na watu wanafiki, akimuweka kwenye nafasi atakapolia na kusaga meno.


Lakini kama mutumishi yule ni mutu mubaya, atajisemesha yeye mwenyewe kwamba bwana wake anakawia,


Nao watumishi wakaenda katika barabara, wakakusanya watu wote waliowaona, wabaya na wazuri, na nyumba ya karamu ikajaa na wageni.


Kisha akawaambia watumishi wake: ‘Karamu ya ndoa iko tayari, lakini si wale walioalikwa ndio waliostahili kuikula.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Na yeyote ambaye hatainama chini na kuiabudu, atatupwa mara moja katika furu la moto mukali.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.


Wanaosingizia wengine wasifanikiwe katika inchi; uovu uwapate watesaji wakali na kuwaangamiza bila kukawia!


Lakini sisi ni sawa na Wayuda wengine; watoto wetu ni sawa na watoto wao. Hata hivyo, tunawalazimisha watoto wetu kuwa watumwa. Wabinti zetu wamoja wamekwisha kuwa watumwa. Hatuna uwezo wa kuzuia jambo hili maana mashamba yetu na mizabibu yetu inanyanganywa na watu wengine.”


Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.


Usimutese mwenzako wala kumwibia. Usikae na mushahara wa mutumishi wako usiku kucha mpaka asubui.


Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Ninyi wabwana muwatendee watumishi wenu kwa usawa na kwa haki, mukijua kwamba ninyi vilevile muko na Bwana wenu katika mbingu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite